chi yamalizika Chelsea 1-3 Liverpool
Dakika ya 90+4: Mechi inamalizika. Mourinho anamsalimia Klopp na kuondoka uwanjani.
Dakika ya 90+2: Zouma anatuma krosi eneo la hatari lakini inapaa juu na kutoka nje.
Dakika ya 90+1: Adam Lallana anaondolewa uwanjani na nafasi yake anaingia Dejan Lovren
Dakika ya 90: Coutinho anashambulia tena. Anapata kona. Mpira unarejeshwa safu ya kati na kisha kwa kipa wa Liverpool.
Image copyrightAP
Dakika ya 82: BAOOOO! Christian Benteke!Chelsea 1-3 Liverpool.
Image copyrightGetty Images
"Utafutwa asubuhi" mashabiki wanaimba wakimkejeli Mourinho. Baadhi ya mashabiki wa Chelsea wanaanza kuondoka uwanjani. Wengine bado wanaimba jina lake.
Dakika ya 80: Chelsea wanashambuliwa tena. Nusura bao liingie.
Dakika ya 75: Alberto Moreno anapata nafasi na kushambulia. Kipa wa Chelsea Begovic anachomoka na kutupa nje kombora lake.
Dakika ya 73: BAOOOOOO! Coutinho! Chelsea 1-2 Liverpool.
Dakika ya 71: Cesc Fabregas anaingizwa nafasi ya John Obi Mikel, huku Chelsea wakiendelea kushambulia.
Dakika ya 70: Chelsea wanapata kona. Inachapwa na Willian lakini haizai matunda.
Dakika ya 68: Lucas Leiva ambaye tayari ana kadi ya njano anamchezea vibaya Ramires. Wachezaji wa Chelsea wanamzingira Mark Clattenburg. Lakini refa hachukui hatua yoyote. Anamuonya tu mchezaji huyo.
Dakika ya 63: Emre Can anapewa kadi ya njano.
Dakika ya 62: Nahodha wa Liverpool James Milner anaondolewa uwanjani na utepe wa unahodha unakabidhiwa Martin Skrtel.
Dakika ya 61: Kenedy nusura afanye mambo. Kenedy anatoa kombora kutoka hatua 18 lakini linaenda nje.
Ramires naye anapata nafasi nzuri lakini mpira wake unazuiwa na Martin Skrtel na Emre Can.
Dakika ya 59: Eden Hazard anatolewa uwanjani na nafasi yake anaingia Mbrazil Kenedy.
Dakika ya 57: Lucas anaonyeshwa kadi ya njano.
Dakika ya 49: Liverpool wanashambulia. Cahill anautoa mpira nje kwa kichwa na inakuwa kona. Tena Cahill anautoa nje wakati huu kwa mguu. Kona nyingine inapigwa lakini kombora la Coutinho linapaa na kupitia juu ya goli.
Dakika ya 49: Ramires anatoka nyuma na kumkabili Coutinho safu ya kati. Refa anatoa frikiki.
Dakika ya 47: Liverpool wanapata nafasi nzuri. Firmino ana mpira, lakini Zouma anaufikia na kuupiga nje.
Dakika ya 46: Chelsea wanashambulia. Lakini kombora la Willian linapinduliwa kisha kunyakwa na kipa.
Mechi inaanza kipindi cha pili.
Ni muda wa mapumziko sasa. Chelsea 1-1 Liverpool
Dakika ya 45+3: BAOOOO! Coutinho anasawazishia Liverpool. Chelsea 1- 1 Liverpool
Image copyrightReuters
Dakika ya 41: Diego Costa anakimbiza mpira eneo la Liverpool lakini unatoka nje kabla yake kuufikia.
Dakika ya 37: Mpira wa mbali unatumwa eneo la hatari la Chelsea. Lucas anaufikia kwa kichwa lakini mpira wake unanyakwa na kipa. Zouma analala chini akionekana kuumia lakini baadaye anainuka na kuendelea na mechi.
Dakika ya 35: Liverpool wanadai Terry amenawa mpira baada ya kutuliza krosi ya Nathani
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni